Dodoma, Jumanne, Januari 31, 2017:
Serikali leo
imeainisha utekelezaji na kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya maendeleo
kwa wananchi katika sekta mbalimbali katika kikao cha kwanza cha Mkutano wa
Sita wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Majibu ya Serikali kwa baadhi
ya hoja ni kama ifuatavyo:
Ujenzi Nyumba za Walimu.
Akijibu
hoja kuhusu ujenzi wa nyumba za walimu, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za
Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo, ameliambia Bunge kuwa Serikali
ilitenga kiasi cha Sh. Bilioni 13.9 katika Bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya
ujenzi wa nyumba za walimu wa Sekondari, na Shilingi bilioni 11.4 kwa nyumba za
walimu wa Shule za Msingi.
Aidha, Waziri
Jafo ameeleza kuwa tayari nyumba 146 za walimu zimeshajengwa nchini kupitia
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari. Pia amezungumzia Serikali kuanza
kulipa madeni ya walimu.
Ujenzi wa Viwanda Nchini
Akijibu
swali kuhusu uwekezaji wa viwanda nchini hususani mkoani Tabora ambako kuna
kilimo cha Tumbaku na maeneo mengine yenye malighafi, Mhandisi Edwin Ngonyani
kwa niaba ya Waziri wa Viwanda ameliambia Bunge kuwa tayari Serikali
imeshafanya mazungumzo na wawekezaji kutoka Vietnam na kuzitaka Halmashauri
zote nchini kuendelea kuitikia wito wa kutenga maeneo ya uwekezaji.
“Kituo
cha uwekezaji Nchini (TIC) kimepewa maelekezo maalum kunadi fursa hii kwa
wawekezaji katika sekta ya tumbaku na sigara hapa nchini,” alisema Mhandisi
Ngonyani ambaye pia ni Naibu Waziri, Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Tupende Bidhaa Zetu.
Akijibu
hoja kuhusu bidhaa nyingi za Kenya kuingia nchini, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Suzan Kolimba amesema moja ya
changamoto inazozikumba bidhaa za Tanzania ni wananchi wake kupenda vya nje.
“Katika
kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali iliunda Kamati ya Kitaifa ya Kudhibiti
na Kusimamia Uondoaji wa wa Vikwazo visivyo vya Kiforodha na kuhamasisha
wafanyabiashara nchini kuzalisha bidhaa zenye ubora,” alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...