Na Amina Kibwana,Globu ya Jamii .

kinara wa Standard Chartered Mumbai Marathon ambaye pia ni Balozi wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Alphonce Simbu amewasili jijini dar es salaam na kueleza yaliyojiri katika mbia hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa habari,utamaduni,Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye ametoa shukurani zake kwa Multichoice Tanzania ambao ni wafadhili wa mwanaridha huyo kwa msaada waliompatia pamoja na pongezi za dhati kwa mwanaridha huyo kuchukua ushindi katika mashindano hayo ambayo yalikuwa na washindani kutoka nchi tofautitofauti,

"Ninawashukuru sana dstv kwa kujitolea kwao pale wanapoona kunafaa kwani mafanikio ya Simbu yamepatikana kwa kupitia msaada huo na kuufanya mchezo huu kurudi tena kwa kasi nchini kulinganisha na awali."

Naye Katibu Mkuu wa chama cha riadha Nchini Willelm Gidabuday amesema kuwa waliamchagua Alphonce kwa kuamini kuwa nanweza na atafanya vizuri katika mchezo huo na kuweza kuiwakilisha vizuri Nchi yetu kutokana na kuweza kufanya vizuri katika mashindano yaliopita.

Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Multichoice Tanzania Ronald Shelukindo amesema kuwa wanaendelea kumdhamini Simbu na kwamba wanatarajia kuwa atafanya vema katika michuano ijayo ya London Marathon ya mwezi April na yale ya Dunia ya mwezi Agosti na kutuwakilisha tena kama alivyofanya huko mumbai nchini India.

"Tunaendela kumdhamini Simbu na tunashirikiana kwa karibu na meneja wake na kocha ili kuhakikisha kijana anajinoa vizuri kwa ajili ya mashindabo yanayomkabili." amesema Ronald.

Kwa upande wake Mwanaridha huyo amewasifu waandishi wa habari kwa kazi walioifanya ya kutoa taarifa kwa umma kuhusu yaliyojiri huko Mumbai wakati wa mashindano hayo pamoja na Ufadhili alioupata kutoka Kampuni ya Multichoice Tanzania kwa kwa kumuwezesha kufanya maandalizi mazuri yenye kiwango kinachohitajika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...