Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Sihaba Nkinga akiwakabidhi Mangariba wastaafu(Kina Mama na Kinababa Wakisasa) vitendea kazi watakavyotumia katika shughuli zao mpya baada ya kuachana na ukeketaji na kuamua kujiwekeza katika ujasiriamali.
Mkurugenzi wa Kituo cha Kulea Watoto waliokimbia Kukeketwa cha (ATFGM-Massanga) Sister Stella Mgaya akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Watoto kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi.Margareth Mussai.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime Bw. Glorious Luoga akiongea wakati wa mahafali ya watoto waliokimbia kukeketwa na kujiunga katika kituo Watoto waliokimbia Kukeketwa cha (ATFGM-Massanga) ambapo aliwataka wazazi wanaowatenga na kuwalazimisha kuwakeketa watoto waliohitumu mafunzo kuacha tabia hiyo kwani watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Sihaba Nkinga akiongea wakati wa mahafali ya watoto waliokimbia kukeketwa na kujiunga katika kituo Watoto waliokimbia Kukeketwa cha (ATFGM-Massanga) ambapo alisisitiza kuwa serikali itaendelea kuwachukulia hatua wazazi na jamii inayoendelea na kitendo kiovu cha ukeketaji kwa watoto wa kike.PICHA NA IDARA YA HABARI .



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...