Waziri wa Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji Mhe,Ali Abeid Amani Karume,alipokuwa akimkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) katika hafla ya Uzinduzi wa Vifaa vipya vya kufanyia kazi Bandarini ikiwemo Makontena na Mizigo mizito leo,ikiwa ni shamra shamra za miaka 53 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akitoa hutuba yake ya Uzinduzi wa Vifaa vipya vya kufanyia kazi katika Bandari ya Malindi Mjini Unguja leo ikiwemo Makontena ya mizigo mizito,ikiwa ni shamra shamra za miaka 53 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,(kulia) Waziri wa Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji Mhe,Ali Abeid Amani Karume,(kushoto) Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe,Balozi Seif Ali Iddi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Bandari Bw.Salmin Senga.
![]() |
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Vifaa vipya vya kufanyia kazi katika Bandari ya Malindi Mjini Unguja leo ikiwemo Makontena ya mizigo mizito wakiwepo na Viongozi mbali mbali, ikiwa ni shamra shamra za miaka 53 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Mashine ya Mobile Harbour Crane LHM 280 yenye uwezo wa kunyanyua Tani 64 ikionesha namna inavyoweza kufanya kazi katika kushusha Makontena katika Meli pia na kupanga sehemu ya kuhifadhia (Container Yard) mara baada ya Uzinduzi wa Vifaa vipya vya kufanyia kazi katika Bandari ya Malindi Mjini Unguja. Picha zaidi BOFYA HAPA
|
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...