Mtoto mwenye ulemavu wa ngozi wa shule maalumu ya msingi ya Mundindi wilayani Ludewa Mkoani Njombe, Yohana Mwaifuge(katikati) akipokea moja ya msaada toka kwa Meneja wa Vodacom Tanzania wa Mkoa huo, Benedict Kitogwa aliyekabidhi msaada huo jana  kwa niaba ya Vodacom Tanzania Foundation.Msaada huo wenye thamani ya shilingi Milioni 15/- ni Vyakula,Sabuni, Magodoro pamoja na mablanketi.
 Meneja wa Vodacom Tanzania Mkoa wa Njombe, Benedict Kitogwa(kushoto) akimsalimia mtoto mwenye ulemavu wa macho wa shule maalumu ya Mundindi wilayani Ludewa Mkoani humo, Robert Lwaizala wakati alipotembelea shule hiyo jana  kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali wenye thamani ya shilingi Milioni 15/- kwa niaba ya Vodacom Tanzania Foundation.
Baadhi ya watoto wanaosoma katika  shule maalumu ya Mundindi wilayani Ludewa Mkoani Njombe, wakila chakula cha mchana na Meneja wa Vodacom Tanzania wa mkoa huo, Benedict Kitogwa(katikati)baada ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali jana kwa niaba ya Vodacom Tanzania Foundation wenye thamani ya shilingi Milioni 15/- kama vile Vyakula, Sabuni, Magodoro pamoja na mablanketi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...