Na Rhoda Ezekiel Kigoma.
CHAMA Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Kasulu Kimemuomba Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Magufuli kuitimiza ahadi yake ya kuwasaidia Wananchi wa Wilaya ya Kasulu ya Kutatua Migogoro ya Mipaka inayo endelea baina ya Wananchi na eneo la hifadhi ya Misitu ya kagerankanda kama alivyo wahahidi Wananchi hao Wakati wa Kampeni kutatua kero hiyo endapo watakichagua Chama hicho.
Akizungumza na gazeti hili katibu mwenezi wa Wilaya ya Kasulu Masoud Kitowe alisema wakati wa kampeni Rais aliwaomba Wananchi hao wakichague Chama cha mapinduzi na kuwaahidi endapo watakichagua chama hicho atahakikisha anatatua mgogoro huo na kuongeza mipaka Kwa Wananchi hao waweze kulima,na Wananchi walikichagua chama hicho mpaka sasa ahadi hiyo haijatekelezwa.
Alisema CCM Wilaya ya Kasulu wanapata shida kuwajibu Wananchi dhidi ya mgoholo unaoendelea katika poli la Kagerankanda Wananchi wanao kutwa Wakilima katika poli hilo wanapigwa na kunyanganywa vifaa vyao kwa madai kuwa hawaruhusiwi kulima katika poli hilo ilihali maeneo ya kulimia katika Wilaya hiyo ni Machache na Wananchi wengi wanategemea kulima Mahindi katika poli hilo.
Kitowe alisema mpaka sasa Dawa zimeshafika katika Wilaya ya Kasulu iliwatu wa TFS waliopewa Dhamana ya kulinda msitu huo wamejipanga kumwagia Tindikari mahindi na Maharage yaliyo pandwa katika poli hilo hali inayoweza kupelekea Wilaya ya Kasulu na wilaya zingine za Mkoa wa Kigoma kukabiliwa na Njaa kwakuwa mazao yanayo limwa katika Msitu huo yanahudumia zaidi ya Wilaya nne za Mkoa wa Kigoma.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...