Na Nteghenjwa Hoseah, Karatu
MKUU wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Mrisho Gambo amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Theresia Mahongo kuhakikisha fedha za walimu wa shule za sekondari na msingi zilizokatwa na halmashauri ya wilaya hiyo kwaajili ya vitambulisho vya kazi zinarudishwa.
Mhe. Gambo alitoa agizo hilo jana wilayani Karatu wakati alipokuwa akizungumza na walimu hao kwenye ukumbi wa shule ya sekondari Karatu Boys ili kujua changamoto wanazokutana nazo na jinsi ya kuzitatua ikiwemo madeni ya likizo, upandaji wa madaraja.
Alihoji ni kwanini walimu hao wakatwe Sh. 6000 kwa ajili ya kutengenezewa vitambulisho vya kazi wakati ni haki yao kama watumishi na waajiriwa wa halmashauri hiyo na ni haki yao kupata vitambulisho vya kazi bure; Mwajiri anao wajibu wa kumtengenezea kila mtumishi Kitambulisho cha kazi. Alimwagiza DC Mahongo kuhakikisha anafuatilia na kumchukulia hatua watumishi wa halmashauri hiyo waliowakata walimu hao wa msingi na sekondari kiasi hicho cha fedha kwa ajili kuwachukulia hatua.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho
Gambo (aliyesimama) akifungua Kikao cha walimu alichokiitisha ili kuskiliza
changamoto zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi wakati wa ziara yake Wilayani
Karatu.
Walimu
wa shule za msingi na Sekondari wanaofanya kazi katika Halmashauri ya Karatu
wakifuatilia kikao kilichoitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha wakati wa ziara ya
kikazi.
1.
Mkuu
wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo akiongea na walimu wa Shule za
Msingi na Sekondari katika Wilaya ya Karatu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...