Askari wa Usalama barabarani jijini Dar es salaam leo wamekamata gari aina ya NOAH ikiwa imebeba watoto 34 pamoja na mwalimu wao na kufanya jumla ya watu 35 katika gari Wanafunzi hao ni wa darasa la kwanza na pili kutoka shule za Diamond, Olympio, Kisutu, Maktaba na Bunge. Gari hiyo imekamatiwa eneo la mzunguko wa  Gerezani  likielekea Vijibweni-Kigamboni.Dereva na wahusika wa gari hiyo wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kwanza wazazi wa hawa watoto wanajua kwamba watoto wao wanasafiri hivi kwenda shule? Kama wanajua ningependa kujua maoni yao. Huu ni uzembe wa hali ya juu, hapa yakitokea ya kutokea watasema ni mpango wa Mungu. Smh.

    Watanzania ifike mahali akili zetu ziamke tuache kusubiri serikali kutufanyia kila kitu na kumsingizia Mungu kwa kila jambo hata kwa yale ambayo tungeweza kuzuia. Mwalimu, dereva, shule na wazazi wachukuliwe hatua kali.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...