Waziri Mkuu, Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa, MB. anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye harambee iliyoitishwa na Shirika lisilo la kiserikali la Land O’Lakes ikilenga kukusanya fedha kwa ajili ya uwezeshaji wa wanawake katika kilimo hasa kilimo biashara nchini kupitia taasisi iliyojikita kwenye kuendeleza wanawake katika kilimo Tanzania (CAWAT).

Akizungumza na waandiishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa Mradi wa Ubunifu  Katika Maswala ya Kijinsia na Kuimarisha Uhakika wa Chakula Katika Ngazi ya Kaya, unaoendeshwa na Land O Lakes, na kufadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Watu wa Merekani (USAID),  Dk Rose Kingamkono, alisema katika harambee hiyo Waziri Mkuu Majaliwa,ataungana na wageni waalikwa wengine zaidi ya 200 na kwamba zaidi ya sh milioni 150 zinatarajiwa kukusanywa.

Alisema lengo la harambee hiyo inayotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam Februari 17 mwaka huu ikiwa na kauli mbiu “WEZESHA KILIMO BIASHARA ILI KUKUZA  AJIRA, JAMII NA VIWANDA ENDELEVU” ni kukusanya kiasi hicho cha pesa kitakachosaidia kuijengea uwezo wa kiutendaji taasisi hiyo mpya ya CAWAT iliyoanzishwa mahususi kusimamia programu endelevu katika kumnyanyua mwanamke kupitia kilimo chenye tija na ufanisi.

“Mwanamke akijengewa uwezo  wa kufanya shughuli za uzalishaji mali kwa ufanisi atakuwa na mchango mkubwa katika kuboresha  ustawi wa familia na jamii kwa ujumla, huku pia akiondoa kabisa tatizo la upungufu wa chakula na lishe duni katika kaya zetu na hayo ndio malengo ya kuanzishwa kwa CAWAT tunayoipigania sasa.

“Tafiti zimeonyesha kwamba uchumi ulioshikiliwa mikononi mwa mwanamke huelekeza matumizi yake kwa ajili ya ustawi wa familia zaidi kuliko ilivyo kwa uchumi ulioshikiwa mikononi mwa mwanaume’’ alisema.

Alisema taasisi hiyo ya CAWAT kwa sasa ipo kwenye mchakato wa awali wa kuanza kujitegemea yenyewe kiuendashaji bila kutegemea msaada iliyokuwa ikiupata kutoka kwenye mradi  unaohusu ‘Ubunifu katika masuala ya kijinsia na kuimarisha uhakikaka wa chakula katika ngazi ya kaya (Innovations in Gender Equality (IGE), to Promote Household Food Security  unaotarajiwa kuisha Machi  mwaka huu.

“Kuelekea katika kujiendesha yenyewe bila kutegemea msaada inayoupata kutoka mradi wa IGE, taasisi hii ya CAWAT bado ina safari ndefu inayohitaji msaada kutoka kwa wadau mbalimbali wa maendeleo ili iweze kutimiza wajibu wake wa kuwasaidia wakina mama walio kwenye sekta hii muhimu ya uzalishaji. Tunawaomba sana  watanzania mmoja mmoja, taasisi, mashirika, balozi mbalimbali waguswe katika kusaidia hili.’’ Alisema.

 Mkurugenzi wa Mradi wa Ubunifu  Katika Maswala ya Kijinsia na Kuimarisha Uhakika wa Chakula Katika Ngazi ya Kaya, unaoendeshwa na taaisisi ya Land O Lakes, na kufadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Watu wa Merekani (USAID),  Dk Rose Kingamkono (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na harambee iliyoitishwa na taasisi hiyo ikilenga kukusanya fedha kwa ajili ya uwezeshaji wa wanawake katika kilimo biashara  kupitia taasisi iliyojikita kwenye kuendeleza wanawake katika kilimo Tanzania (CAWAT). Wengine ni maofisa wa taasisi hiyo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...