Mkuu wa wilaya ya Mbinga Mhe. Consimas
Mshenyi (pichani) amewataka wananchi wilayani humo kuhakikisha wanatunza ziada ya chakula
walichonacho kutokana na hali ya mvua kutoridhisha licha ya kusema hakuna njaa katika wilaya
yake.
Akitoa taarifa mbele ya
waandishi wa habari kuhusu hali ya chakula katika wilaya hiyo mkuu huyo wa
wilaya amesema mpaka sasa vituo vya hifadhi ya chakula wilayani hapo vina zaidi
ya tani 300 huku ziada kutoka kwa wananchi ikiwa ni tani 10,000 za
mahindi huku mchele ikiwa ni tani 18,000.
“Nawataka wananchi
waendelee kuhifadhi ziada ya chakula walichonacho kwani hali ya mvua si nzuri
na ziada hiyo inaweza kupungua pia ziada hiyo inaweza saidia hata kwa majirani
zetu” alisema DC Mishenyi.
Aidha Mhe. Mishenyi alisema kuwa
hali mazao yaliyopo shambani yapo katika hali nzuri licha ya mvua kunyesha
katika hali ya kutoridhisha lakini kuna uhakika wa mazao hayo kukomaa na
kuvunwa kwa wakati hivyo akawataka wananchi hususani wakulima kuhakikisha
wasimamia utanzaji kwa kushirikiana na wataalamu wa kilimo
Katika hatua nyingine mkuu
huyo wa wilaya amepiga marufuku unywaji na uuzwaji wa pombe nyakati za kazi
kwani kunazoletesha maendelea ya nwilaya hiyo “sitawavumilia wanaokunywa saa za
kazi na wanaocheza pool table nyakati za
mchana yaani saa za kazi nitawamuagizaa kupitia kwa afisa biashara mkurugenzi
kufuta leseni kwa wale vwote watakao kiuka mashart ya biashara zao ikiwemo
kuuza pombe katika saa za kazi”
Kuhusu uchaguzi mdogo wa
udiwani utakaofanyika Januari 22 mwaka huu
katika kata ya maguu wilayani hapa Mishenyi amewataka wanachi kupiga kura kwa amani na kurejea makwao kusubiri matokeo, huku akiwaomba wagobea kutokuwa vyanzo
kuvuruga amani na utulivu na kuwahakikishia ulinzi wa kutosha katika uchaguzi
huu
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...