Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (kulia),
akipeana mkono na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB),
anayeshughulikia masuala ya Nishati na Mabadiliko ya Tabianchi, Bw.
Amadou Hott, (kushoto) baada ya kumalizika kwa mkutano kati yao kuhusu
ahadi zilizotolewa na Benki hiyo katika kuchangia maendeleo ya Tanzania
kwa njia ya ruzuku na mikopo yenye masharti nafuu, katika ukumbi wa
Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), (Katikati) akiwa katika mkutano na ujumbe wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), ukiongozwa na Makamu wa Rais wa Benki hiyo anaye husika na masuala ya Nishati na Mabadiliko ya Tabia Nchi, Bw. Amadou Hott, na Ujumbe kutoka Tanzania, ambapo masuala kadhaa kuhusu uchumi, Nishati, Kilimo, Teknolojia jadidifu, yamezungumzwa ili kukuza uchumi wa nchi, Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam
Wajumbe wa mkutano wa kujadili ahadi zilizotolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), kutoka Benki hiyo na Tanzania wakifuatilia maelezo kutoka kwa Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), (hayupo pichani) kuhusu umuhimu wa AfDB, katika utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Khamis Shaaban (kulia), Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara hiyo Bw. John Rubuga (katikati) na Afisa Mwandamizi wa Wizara Bw. John Mavura wakifuatilia mjadala kuhusu ahadi zilizotolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), katika kufanikisha maendeleo ya Tanzania, katika ukumbi wa Wizara hiyo Jijini Dar es Salaam..
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), anayeshughulikia masuala ya Nishati na Mabadiliko ya Tabia nchi, Bw. Amadou Hott, wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wengine baada ya kumalizika kwa mkutano kuhusu ahadi zilizotolewa na Benki hiyo juu ya maendeleo ya Tanzania katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM) .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...