Na Rhoda Ezekiel-Globu ya Jamii, Kigoma.

JESHI la polisi Mkoani Kigoma linamshikilia mtu Mmoja kwa kosa la kukutwa na vipande vitatu vya Pembe za ndovu vyenye uzito wa kilo 15 vyenye thamani ya shilingi za kitanzania Milioni 500 akivisafirisha kutoka Katavi kuvileta kigoma kwa ajili ya kuviuza.
Sambamba na tukio hilo jeshi la polisi linawashikilia Wahamiaji halamu 231, Bangi keye 220, mtambo Mmoja wa kutengenezea pombe ya moshi na watuhumiwa 10 wakiwa na lita 217 , watuhjmiwa hao ni wauzaji na wapikaji kitendo ambacho ni kinyume na sheria za Nchi.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jana ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa Wa Kigoma Naibu kamishina Wa Jeshi la polisi , Fredinandi Mtu alisema mnamo tarehe februali6 mwaka majira ya saa sita huko katika Kijiji Cha Kazuramimba Wilayani Uvinza Askari walipokea taarifa kuwa kuna wizi umetokea Katika Gari ya Saratoga Iliyokuwa ikitokea Tabora kuja Kigoma , askari Walifanya upekuzi na kukamata begi la abiria mmoja jina lake limehifadhiwa kwaajili ya upelelezi likiwa na vipande vitatu vya meno ya tembo.
Kamanda Mtui alisema Upelelezi wa tukio hilo unaendelea ilikufahamu mahali mtuhumiwa alipotoa vipande hivyo vya meno ya tembo , Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani pindi upelelezi utakapo kamilika kwa hatua zaidi za kisheria.
"Jeshi la polisi Mkoani Kigoma tunawaomba Wananchi Kuendelea kuunga Mkono jitihada za vita dhidi ya uhalifu kwa kutoa taarifa za watu wanao jihusisha na vitendo hivyo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao na kukomesha vitendo hivyo.
Kwa upande wake Afisa Wanyamapori Wilaya ya Kigoma, Iddi Salumu alisema katika Mapori ya Kigoma hakuna pembe za ndivu za aina hiyo zilizo kamatwa vipande hivyo vinaweza kuwa vimetokea katika Mkoa Wa Katavi au katika hofadhi ya TANAPA ya Seruu .
Alisema Kigoma Ndio njia kuu ya Kupitishoa mozigo hiyo na biashara kubwa inafanyikia Bchini Burundi , kwa Nchi ya Burundi biashara hiyo imeruhusiwa na majangiri wengi wanatumia Njia ya Mkoa Wa Kigoma kupitishia mizigo hiyo.
Salumu alisema katika kuhakikisha biashara hiyo inadhibitiwa wameamua kuboresha Doria kwa kushirikiana na Jeshi la polisi na polisi waliopo Mipakani ilikuweza kudhibiti na kufanya ukaguzi wa mizigo yote inayopita kuelekea Nchini Burundi.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...