Na Mr. Pengo, MMG
BODI ya Shirika la Madini Tanzania (STAMICO) limesema limejipanga kuhakikisha linafufua shughuli za uchimbaji wa makaa ya mawe katika mgodi wa Kiwira coal mine uliosimama kwa zaidi ya miaka nane.
Hayo yalibanishwa katika Ziara ya Wajumbe wa Bodi ya STAMICO katika migodi ya Kabulo na Kiwira iliyoko Wilaya ya Ileje mkoani Songwe iliyofanyika juzi kwa lengo la kujionea hali ilivyo.
Akizungumza katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa Bodi, Balozi Alexander Muganda alisema bodi iliundwa Julai mwaka jana na imefanya zioara ya kutembelea miradi yote iliyochini ya Stamico ili kuona namna ya kuiendesha kwa manufaa.
Alisema kuhusu Mgodi wa Kiwira na Kabulo, Bodi imeona jinsi itakavyoweza kuishauri Menejimenti ili iweze kuanza kuchimba makaa yam awe kwa ajili ya kuuza na mpango wa baadaye uwe kuzalisha umeme.
Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Stamico, Mhandisi Said Mkwawa alisema bodi imeona mradi ulivyo na jinsi ya kufanya uwekezaji ili shirika liweze kujiendesha kwa tija.
Alisema bodi imegundua kuwa makaa ya mawe katika mgodi wa Kiwira na Kabulo unapatikana juu juu hivyo shirika haliwezi kutumia gharama kubwa ya kuanza uchimbaji na kwamba hadi sasa kuna hazina ya tani milioni 40 hadi 50.
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Luten Mstaafu Chiku Galawa akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Madini Tanzania (STAMICO) Balozi Alexandekwake kabla ya kufanya ziara katika migodi ya makaa ya mawe ya Kiwira na Kabulo.
Mwenyekiti wa Bodi ya STAMICO, Balozi Alexander Muganda akitoa taarifa kwa Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya kuhusu Ziara ya Bodi kutembelea migodi ya Kabulo na Kiwira coal mine
Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Kiwira, Mhandisi Aswile Mapamba akitoa maelezo kwa wajumbe wa bodi ya Stamico kuhusu mgodi wa Kabulo uliopo Ileje mkoani Songwe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...