Timu ya  Cameroon ya safari hii ilikuwa mbovu katika historia. Angalau ndivyo walivyoonekana wiki mbili na nusu zilizopita, lakini mpira unadunda. Lolote laweza kutokea. Na baada ya wachezaji nyota wanane kujitoa kutokana na kocha wao Hugo Broos kusisitiza nidhamu, majina mengine  makubwa yakawekwa benchi. Lakini kikosi chake kilichokuwa na uzoefu mdogo kilifanya makubwa na hata kuweza kusawazisha na hatimaye kuishinda Misri kuipanchi hiyo ushindi wa mara ya tano wa kombe hilo la AFCON, na  kwanza  katika kipindi cha miaka 15.
Majina makubwa ndiyo yaliyorejea uwanjani na kuwezesha ushindi huo, magoli yote yakiwa yamefungwa na wachezaji wa akiba. Mohamed Elneny aliipatia Misri bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza lakini Nicola Nkoulou alisawazisha kabla bao la ushindi kuwekwa kimiani na Vincent Aboubakar zikiwa zimesalia dakika mbili mchezo umalizike. Hakika lilikuwa goli tamu.
Msisimko ulikuwa mkubwa mno uwanjani wakati raia wa Cameroon wanaoishi Gabon walipojitokeza kwa maelfu kushangilia vijana wao, huku mabasi kibao yaliyosafiri usiku kucha  kutoka Doula na Yaounde yakileta mashabiki zaidi, na kwa mara ya kwanza uwanja wa L'Amitie ulifurika kwa mara ya kwanza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...