Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI,Selemani Jafo,amesema mkoa wa Pwani umepokea Bil.2.340 zitakazotumika kugawanywa kwenye vituo vya afya na zahanati 234 zilizopo mkoani hapo ili kuboresha na kutatua changamoto zilizopo.
Amesema fedha hizo zimetolewa kutoka katika mpango wa malipo kwa ufanisi unaotekelezwa kwa ushirikiano baina ya bank ya dunia na serikali ya Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.Aidha Jafo amewasihi wakurugenzi,wenyeviti wa halmashauri na mganga mkuu wa mkoa huo,kusimamia fedha hizo ili ziweze kuleta tija .
Katika hatua nyingine,ametoa wiki moja hadi kufikia februari 21 mwaka huu,kwa waganga wakuu wa mikoa (RMO)na makatibu tawala wa mikoa (RAS)kote nchini,kuhakikisha wanapeleka account za bank zinazotumiwa katika vituo na zahanati zote.Alhaj Jafo,aliyasema hayo wakati akizungumza na wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri pamoja na waganga wakuu wa wilaya mkoani Pwani.
Alisema kati fedha hizo kila zahanati na kituo cha afya kitapatiwa kiasi cha sh.mil 10 ili kuboresha na kutatua kero sugu zilizokuwa zikiwasumbua.“Kuna zahanati na vituo vya afya ambavyo havina magodoro,mapaa yamebomoka,,hakuna vyoo huku nyumba za mganga wa kituo nayo ikiwa haina choo”“Kuna maeneo mengine hayana hata vitanda vya kujifungulia,akinamama wanapata shida yaani unahofia wanaweza kuondoka hata na magonjwa mengine,hivyo kwa mazingira haya fedha hizi endapo zitatumika kikamilifu zitaondoa matatizo hayo”alisema Jafo.
Alisema katika miaka iliyopita fedha hizo zilikuwa hakuna hivyo kutokana na mpango huo kuanza,wahakikishe wanaleta matokeo chanya kwa kujibu changamoto zilizokuwa zikiwakabili.Jafo alisema hatofurahishwa akisikia mradi huo haujafanikiwa katika mkoa wa Pwani na mikoa mingine 8 ambayo ipo kwenye mradi huo kwa majaribio hapa nchini.
NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI,Selemani Jafo,akizungumzia na wakurugenzi,wenyeviti wa halmashauri,waganga wakuu wa wilaya mkoani Pwani,jana.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...