Na
Bashir Yakub.
Sheria
inayoshughulikia habari nzima
ya madawa ya
kulevya inaitwa “The Drug
Control And Enforcement
Act”. Ni sheria
namba 5 ya
mwaka 2015. Ni
sheria mpya kabisa. Msanii Wema
Sepetu ni kati
ya Watu walioko
mahakamani tayari kuamuliwa
kwa mujibu wa
sheria hii.
1.AINA YA
DAWA ZA KULEVYA.
Sheria hii inataja
aina nyingi mno
ya vitu ambavyo
imeviita dawa za
kulevya. Vipo jamii ya kimiminika, jamii
ya unga, jamii
ya miti, majani, mbegu
n.k.
Kifungu cha 2
cha sheria hiyo
kinachosomwa sambamba na Schedule
ya 1 ya sheria
hiyohiyo kimeorodhesha zaidi
ya sampuli 100
ya vitu ambavyo
vinahesabika kuwa ni
dawa za kulevya hapa
Tanzania. Humo imo pia
bangi, mirungi, cocaine, heroine
na aina
nyingine nyingi. Katika
hizi Msanii Wema
anatuhumiwa kukutwa na
misokoto ya bangi.
2. JE
ILIKUWA SAWA WEMA
KUPEWA DHAMANA ?.
Ndio ilikuwa sawa. Wako
watu wanasema kuna
mtu amemkingia kifua
akapata dhamana. Hili si kweli .
Dhamana katika kesi
za madawa ya
kulevya hunyimwa kutokana
na kiwango ulichokutwa au unachotuhumiwa nacho.
Kifungu cha 29
cha Sheria hiyo
ya kupambana na
dawa za kulevya
kimeeleza hilo kama
ifuatavyo;.
( a ) Kama
ni cocaine, heroine, mandrax,
morphine, cannabis resin au opium
kuanzia gramu 200 au
zaidi hakuna dhamana.
Ni pote polisi
na mahakamani.
( b ) Kama
ni dawa aina
ya majani au
mimea kama bangi n.k
kuanzia kilo 100
au zaidi hakuna
dhamana. Ni pote polisi na
mahakamani.
( c ) Kama
ni dawa zenye
mfumo wa kemikali
kuanzia lita 30 au
zaidi au kilo 100
ikiwa zimewekwa katika
mfumo wa unga au
vinginevyo hakuna dhamana.
Ni pote polisi na
mahakamani.
Wema Sepetu alikutwa
na kiwango kidogo kwa taarifa
zilizotolewa, ni kama
msokoto mmoja hivi.
Ukiangalia hapa juu
hakuna popote ambapo kiwango hicho
kimetajwa kuwa hakidhaminiki. Kwa
hiyo kosa lake
lilikuwa la kudhaminika
kabisa kwa mujibu
wa kifungu hiki.
3. JE
WEMA ANAKABILIWA NA
ADHABU ZIPI ?.
Kifungu cha 17 ( 1 )
cha Sheria ya
Kuzuia na Kupambana
na dawa za
kulevya kinaeleza adhabu
ya miaka mitatu
jela, au faini isiyopungua
laki tano au
vyote viwili.
Kwahiyo panapo kupatikana
na hatia atatakiwa
kwenda jela miaka
mitatu, au asiende
jela iamuliwe alipe
faini inayoanzia laki
tano za Tanzania,
au aende jela
miaka mitatu na
hapohapo alipe na faini
inayoanzia shilingi laki
tano kwenda mbele.
KUSOMA ZAIDI
sheriayakub.blogspot.com.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...