Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imekutana nakufanya kikao na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kupokea taarifa ya maendeleo ya miradi ya TPDC mjini Dodoma.
Wataalam wa TPDC katika kikao hicho walipata fursa ya kuwasilisha mada za taarifa ya maendeleo ya miradi ya Shirika hilo.
Aidha, katika kikao hicho Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPDC Prof. Sufian Bukurura na Mkuu wa Taasisi ya Utafiti (REPOA) Dk. Donald Mmari waliwasilisha mada kuhusu utafiti walioufanya kuhusu Shirika la Mafuta la Taifa linavyoweza kujiendesha kwenye mazingira ya sheria mpya nchini.
Akihitimisha kikao hicho Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, Mhe. Naghenjwa Kaboyoka alisema kuwa Kamati yake imepokea taarifa ya maendeleo ya miradi ya TPDC na kwamba Kamati itakaa nakuifanyia kazi.
  Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. Naghenjwa akifungua kikao kulichoikutanisha Kamati ya PAC na TPDC mjini Dodoma
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPDC, Prof. Sufian Bukurura akiwasilisha mada mbele ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) katika kikao kilicho ikutanisha Kamati hiyo na TPDC mjini Dodoma.
  Mkuu wa Taasisi ya Utafiti (REPOA) Dk. Donald Mmari akiwasilisha Mada mbele ya Kamati ya PAC mjini Dodoma
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wakimsikiliza mtoa mada kutoka TPDC katika kikao hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...