Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akipokelewa na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza alipowasili Makao Makuu ya Jeshi hilo baada ya kuapishwa rasmi kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Ikulu Jijini Dar es Salaam Februari 6, 2017.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akipokea salaam ya heshima toka katika Gwaride Maalum lililoandaliwa na Maofisa na askari(hawapo pichani) kwa ajili yake kwa heshima.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akikagua Gwaride Maalum lililoandaliwa na Maofisa na askari wa Jeshi la Magereza kwa ajili yake kwa heshima kama inavyoonekana katika picha.
Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza, Gaston Sanga(kulia) akiteta jambo na Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa kabla ya kuongea na Maafisa na askari wa Jeshi hilo Makao Makuu ya Magereza mara baada ya kutoka kuapishwa kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza.
Baadhi ya Askari wa Jeshi la Magereza wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa mara baada ya kutoka kuapishwa kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Ikulu Jijini Dar es Salaam Februari 6, 2017.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...