Ujumbe wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL Limited) uliwasili Visiwani Komoro tarehe 5 February, 2017. Ujumbe huo ukiongozwa na Bw. Emmanuel Korosso ulipokelewa na Mhe. Chabaka Kilumanga, Balozi wa Tanzania, Visiwani Komoro. Aidha Mwenyekiti huyo aliongozana pia na Bw. Ladislaus E. Matindi Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL. 

Madhumini ya ziara hiyo ilikuwa ni kuja kuangalia namna gani ATCL inaweza kutanua wigo wa safari zake Visiwani Komoro. Hii ikiwa ni sehemu ya mkakati wa shirika hilo kuweza kulidhibiti kikamilifu soko la anga la Visiwa vya Komoro ambapo kwa sasa Soko hilo limekuwa na ushindani mkubwa kutoka kwa mashirika mengine ya Kimataifa kama vile  Ethiopian Airlines, Air Madagscar, Kenya Airways n.k.

Katika ziara hiyo, wajumbe walipata fursa ya kuongozana na Mhe. Balozi kwenda Kisiwa cha Anjoun na kufanya mazungumzo na Gavana wa Kisiwa hicho Mhe. Abdou Salami Abdou. Ifahamike kwamba Shirika la ndege la ATCL hufanya safari zake mara tatu kwa wiki Visiwani Komoro ambapo ndege hiyo hutua katika uwanja wa Kimataifa wa Prince Said Ibrahim Jijini Moroni. 

Komoro ni Muungano wa Visiwa Vitatu ambavyo ni Anjoun, Ngazidja na Moheli.  Hata hivyo imeonekana kuwa abiria wengi wanaosafiri kuja Tanzania kwa ajili ya shughuli za biashara hutokea Katika Kisiwa cha Anjoun.  Imejidhihirisha kuwa  abiria kutoka Ksiwa cha Anjoun hupata usumbufu kwa vile hakuna safari za moja kwa moja kutoka Kisiwa hicho kwenda Dar es Salaam, hali ambayo imeonekana kuongeza ghara za usafiri kwa abiria hao.

Aidha katika mazungumzo yao na Gavana wa Kisiwa cha Anjoun ujumbe huo uliwasilisha maombi ya ATCL kupewa kibali cha kutua Kisiwa cha Anjoun ambapo Gavana huyo aliridhia maombi hayo na kueleza kufurahishwa kwake na dhamira ya ATCL kufanya safari zake Kisiwani hapo. 
 Bw. Ladislaus Matindi akisamilimiana na Gavana wa Anjoun Mhe. Abdou Salam Abdou
  Mazungmzo yakiendelea katika ofisi ya Gavana
 Mhe Balozi akilakiwa na viongozi mbalimbali wa Kisiwa
 Mhe Balozi akiongoza kikao na wadau wa biashara kutoka Kisiwa cha Anjoun.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...