Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisaini kitabu cha maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa UWT, Tawi la Shirikisho la Wanafunzi vyuo vya Elimu ya Juu-CCM, Anastazia Malamsha, wakati wa mazishi ya kiongozi huyo, yaliyofanyika leo katika eneo la  Shimbo, Rombo Mkuu mkoani Kilimanjaro. Anastazia alifariki dunia Jumapili, Feb 5, 2017,  katika ajali ya gari wakati akitoka kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 40 ya CCM mkoani huo ambapo pamoja naye viongozi wengiewatatu walifariki pia katika ajali hiyo.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa salama za rambirambi za kwake binafsi, CCM na Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli wakati wa mazishi hayo
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoaheshima za mwisho kwa mwili wa Anastazia, kabla ya mazishi hayo.
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiweka udongo kaburini wakati wa maziko.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiweka shada la maua kwenye kaburi la Anastazia, mwishoni mwa maziko.PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO
 Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, wakiwa kwenye mazishi hayo. Anastazia alikuwa mwanafunzi wa Mwaka wa tatu katika chuo hicho Kikuu cha Ushirika Moshi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...