Na Ismail Ngayonga, MAELEZO, Mwanza
MAAFISA Habari na Mawasiliano katika sekretarieti za Mikoa na Halmashauri za Wilaya nchini wametakiwa kujitokeza na kuwajibika kikamilifu ili kuwawezesha waaajiri wao kutambua wajibu na majukumu yao ya msingi katika kutangaza shughuli na mafanikio ya Serikali katika maeneo yao ya kazi.
Rai hiyo imetolewa leo Jijini Mwanza na Mkurugenzi wa Habari na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas wakati alipokuwa akizungumza na Maafisa Habari na TEHAMA katika mafunzo elekezi ya tovuti yanayofadhiliwa na Shirika la Misaada la Marekani (USAID) na kusimamiwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na Wakala ya Serikali Mtandao (EGA).
Kwa Mujibu wa Dkt. Abbas alisema katika ulimwengu wa sasa suala la teknolojia ni jambo lisiloupekika, hivyo ni wajibu wa Afisa Habari kutmia nyenzo za kisasa za mawasiliano ikiwemo tovuti ili kuhakikisha kuwa wananchi na wadau wa maendeleo wanapata taarifa sahihi na zilizozingatia wakati.
“Zipo taarifa za miradi mbalimbali ambayo Serikali imeifanya, pamoja na taarifa za bajeti za halmashauri ambazo wananchi watapenda kuzifahamu, hivyo ni wajibu wenu Maafisa Habari kuweka taarifa hizi” alisema Dkt. Abbas.
Aidha aliongeza kuwa ni wajibu wa kila Afisa Habari aliyopo katika Mkoa na Halmashauri nchini aweze kujiwekea malengo ya utekelezaji ili aweze kujitafakari kwa kuwa kuwa kupitia malengo hayo ataweza kutatua changamoto mbalimbali zinazomkabili katika eneo lake la kazi.
Akifafanua zaidi Dkt Abbas alisema ili kufikia malengo hayo Maafisa HabariHabari hawana budi kutengeneza mtandao wa mawasiliano baina yao ili kuwawezesha kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili katika maeneo yao ya kazi.
Dkt. Abbas alisema Serikali inatambua changamoto mbalimbali zinazowakabili maafisa Habari katika maeneo yo ya kazi, ambapo baadhi ya changamoto hizo zimeanza kupatiwa ufumbuzi ikiwemo suala la miongozo ya majukumu ya Afisa Habari na Mawasiliano.
Kwa Upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Rebbeca Kwandu alisema katika mafunzo hayo yaliyotolewa kwa Maafisa Habari na TEHAMA yatasaidia kwa kiasi kikubwa kujibu hoja na kero mbalimbali za wananchi ambazo zimekuwa zikiwasilishwa mara kwa mara katika halmashauri mbalimbali nchini.
“Afisa Habari atakuwa ndiye mhusika wa karibu zaidi atayekuwa akiweka maudhui ya tovti hizi lakini pia Afisa TEHAMA yeye atawajibika kwa kiasi kikubwa katika eneo la la ufundii” alisema Kwandu.
Naye Afisa Habari wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, John Mlyambato alisema baadhi ya Mikoa nchini ikiwemo Mkoa wa Tabora kwa kipindi umekuwa hauna watumishi wa kada ya Maafisa Habari hatua inayosababisha taarifa mbalimbali za Serikali kutowafikia kuwafikia wananchi.
Mkurugenzi wa Habari na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas
akizungumza na Maafisa Habari na Tehama wakati wa Mafunzo elekezi ya matumizi
ya tovuti katika Mikoa na Halmashauri za Wilaya nchini yaliyofadhiliwa na
Shirika la Misaada la Marekaani (USAID) na kusimamiwa na Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Wakala ya Serikali Mtandao. Mafunzo hayo
yalianza tarehe 9-20 Februari, 2017, kulia ni Mkuuwa Kitengo cha Mawasiliano
Ofisi ya Rais TAMISEMI, Rebecca Kwandu.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...