Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imefanya Mnada wa pili wa
kimataifa wa madini ghafi ya Tanzanite kuanzia tarehe 9 – 12 Februari
2017. Mnada huo umefanyika katika kituo cha Jemolojia (TGC) kilichopo
jijini Arusha.
Kampuni tatu zinazochimba madini ya Tanzanite ambazo ni Tanzanite
One Mining Company Ltd, Mathias J Lyatuu Mining na Tanzanite Africa
Ltd; zilileta jumla ya gramu 990,444.04 za madini ghafi kwenye mnada
huo kwa ajili ya mauzo.
Baada ya taratibu za mnada, jumla ya gramu 990,039.04 za Tanzanite
ghafi ziliuzwa kwa Dola za Marekani 4,202,287.13. Hii ni sawa na
99.9% ya madini yote yalilyoletwa kwa ajili ya mauzo. Kutokana na
mauzo hayo, Serikali inatarajia kukusanya mrabaha wa Dola za
Marekani 210,114.36 sawa na Shilingi 466,453,871.43. Aidha,
Halmashauri ya Wilaya ya Simajiro inatarajia kulipwa Shilingi
27,987,232.29 kama Kodi ya Huduma.
Kampuni 68 kutoka nchi saba duniani ambazo ni Tanzania, Kenya,
India, Sri Lanka, China, Uswisi na Ujerumani zimeshiriki katika mnada
huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...