Jeshi la Polisi kanda Maalum ya Dar es Salaam limeendeleea kuwashikilia Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusufu Manji na Askofu Josephat Gwajima kwa zaidi ya saa 24 mpaka sasa.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo, Kamanda wa Polisi kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Siro amesema kuwa watu hao jana walifika hapo na kukutana na wapelezi .

“watu hawa wamehojiwa kuanzia jana mpaka saa za usiku kisha wakawekwa mahabusu  hivyo mpaka sasa ninavyozungumza wapo mahabusu wakisubiri utaratibu mwingine” amesema  kamanda Siro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...