Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam,Paul Makonda amewataja watuhumiwa 65 wa Dawa za Kulevya. Katika majina hayo ametajwa Freeman Mbowe, Mchungaji Gwajima, Yusuf Manji na mbunge mstaafu Idd Azzan.

Akizungumza na waandishi wa habari Ofisi kwake mapema leo jijini Dar,RC Makonda ameingia katika awamu ya pili ya kutaja majina hayo na kuyaweka hadharani,huku akieleza kuwa watuhumiwa hao watatakiwa kufika kituo cha polisi kati siku ya Ijumaa,saa tano asubuhi kwa mahojiano zaidi.
Katika hatua nyingine RC Makonda amekiri kukamatwa kwa Mmiliki wa kituo cha Radio ya EFM, ajulikanae kwa jina la Francis Ciza, almaarufu kwa jina la Dj Majay."tulipokuwa tukifanya opereseheni ya kuwakamata Wahusika wote wa Dawa za kulevya juzi usiku nae akakamatwa kwa mahojiano zaidi;"alisema Makonda.
Makonda amejibu habari za kukamatwa kwa Dj Majay mara baada ya kuulizwa swali na mmoja wa waandishi wa habari, kufuatia tetesi nyingi zilizokuwa zikisambazwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii.
Soma zaidi majina ya watuhumiwa wa sakala hilo la Dawa za kulevya.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. ukisoma vizuri kwenye list SIO FREEMAN MBOWE ni PHILEMONI MBOWE ambaye ni mtu tofauti....

    ReplyDelete
  2. mtoa maoni Sakaya :usijaribu kupotosha ukweli sikiliza video ya majina yanayotajwa ni Mbowe gani aliyetajwa ! jibu ni mbunge wa Hai,sasa yupi?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...