SERIKALI ya Uholanzi imeingiza nchini aina 14 ya mbegu za viazi kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa zao hilo na kuboresha maisha ya wakulima kupitia mradi wa kuboresha zao la viazi nchini.

Akizungumza katika kikao cha ufunguzi wa mradi huo kilichofanyika mkoani Morogoro katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) jana, Mshauri wa Kilimo wa Ubalozi kwa nchi za Kenya na Tanzania, Bw. Bert Rikken alisema nchi yake imeona Tanzania ina nafasi kubwa ya kuongoza uzalishaji wa viazi kutokana na ukubwa wa ardhi na hali ya hewa.

Bw. Rikken alibainisha wameamua kuingiza mbegu hizo ili kuongeza uzalishaji kwa sababu wakulima wanazalisha chini ya tani nane hadi 10 kwa hekta, hivyo ujio wa mbegu hizi utasaidia kuongeza uzalishaji na kufikia tani 40 kwa hekta.

“Mbegu hizi ni nzuri kwa matumizi mengi, viazi vyake vina ladha nzuri na vinaweza kutumika kutengeneza chips au bidhaa nyingine zitokanazo na viazi ambazo zinaweza kusafirishwa nje ya nchi. Mradi huu ulianza kwa kutiliana saini mawaziri wa kilimo kutoka Tanzania na Uholanzi mwaka 2016 ili kuruhusu mbegu kuingia nchini ili kupata ithibati,” alisema Rikken.

Mradi huo wa miaka mitatu utakaogharimu kiasi cha Euro 388,000 sawa na Sh milioni 700, utahakikisha Tanzania inapata mbegu mpya za zao hilo na kutoa mafunzo kwa taasisi zinazojihusisha na kilimo nchini ili kuongeza uzalishaji.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Programu ya Kuendeleza Kilimo Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), Bw.Geoffrey Kirenga  akisisitiza  jambo wakati wa warsha ya siku moja juu ya zao la viazi nchini na namna ya kuliongezea thamani. Kushoto ni Naibu Ofisa Mtendaji Mkuu wa SAGCOT, Bi. Jennifer Baarn, wapili kushoto ni Mshauri Mwandamizi wa Kimataifa  wa maswala ya Mbegu toka Uholanzi,Bw.Jos van Meggelen na kulia ni Kaimu Mthibiti Mkuu wa Mbegu toka Taasisi ya Udhibiti wa Mbegu nchini(TOSCI),Dr.George Swella. Warsha hiyo iliwakutanisha wadau wa kilimo cha viazi toka Tanzania na Serikali ya Uholanzi.
 Baadhi ya washiriki waWarsha  iliyowakutanisha wadau wa kilimo cha viazi toka Tanzania na Serikali ya Uholanzi wakifurahi kwa kushikana mikono kuashiria ushirikiano kati ya nchi hizo mbili katika kukuza na kuliongezea thamani zao la viazi nchini. Warsha hiyo ilifanyika Mkoani Morogoro katika ukumbi wa Taasisi ya Uthibiti wa Mbegu Nchini(TOSCI).
 Afisa kilimo toka ubalozi wa Uholanzi Nchini,Bi.Theresia Mcha(kulia) akijadiliana jambo na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Programu ya Kuendeleza Kilimo Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), Bw.Geoffrey Kirenga mara baada ya kumaliza warsha ya siku moja juu ya zao la viazi nchini na namna ya kuliongezea thamani. Kushoto ni Naibu Ofisa Mtendaji Mkuu wa SAGCOT, Bi.Jennifer Baarn na wapili kushoto ni Mkuu wa maendeleo ya kongani toka SAGCOT, Bi. Maria Ijumba. Warsha hiyo iliwakutanisha wadau wa kilimo cha viazi toka Tanzania na Serikali ya Uholanzi.

Baadhi ya washiriki wa Warsha iliyowakutanisha wadau wa kilimo cha viazi toka Tanzania na Serikali ya Uholanzi wakiwa katika picha ya pamoja. Walijadili pia namna ya kukuza na kuliongezea thamani zao la viazi nchini. Warsha hiyo ilifanyika Mkoani Morogoro katika ukumbi wa Taasisi ya Uthibiti wa Mbegu Nchini(TOSCI).

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...