Mwenyekiti wa Tamasha la Busara Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akiwa na Mabalozi wa Norway na Uswisi kulia kwa Mhe Simai ni Balozi wa Uswisi Tanzania Balozi Florence Tinguely na Balozi wa Norway Tanzania Balozi Hanne Marie wakiangalia wakiangalia vikundi vya Utamaduni wakati wa Uzinduzi wa Tamasha la Sauti za Busara katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Kisongo leo wakiangalia burudani hizo.
Wasanii wa Kikundi cha Utamaduni kutoka Nchini Burundi wakitowa burudani kwa Wananchi wa Zanzibar katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Zanzibar kabla ya kuaza kwa maandamano ya Uzinduzi huo yalioazia katika viwanja hivyo hadi katika viwanja vya bustani ya forodhani.
Wasanii kutoka burundi wakionesha umahiri wao wa kupiga ngoma za utamaduni wa Kwao.
Wasanii wakitowa Burudani katika Viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Kisonge.
Wanafunzi wa Skuli ya Maandalizi Jangombe wakicheza ngoma ya Bomo katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu kabla ya kuaza kwa maandamano ya Uzinduzi wa Tamasha la Busara Zanzibar.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...