SIMU.TV: Mkuu wa mkoa wa Dar, Paul Makonda ametaja majina mengine ya watuhumiwa wa dawa za kulevya wakiwemo wanasiasa, viongozi wa dini na wafanyabiashara; https://youtu.be/FdThrDlJWiU

SIMU.TV: Kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar Es salaam Simon Sirro amesema polisi wanaendelea na uchunguzi kuwabaini watuhumiwa wa dawa za kulevya; https://youtu.be/ZWAQHrZa2v0

SIMU.TV: Rais Dkt John Magufuli amefanya ziara ya kushtukiza katika eneo la ujenzi wa jengo jipya la uwanja wa ndege na kuagiza kazi iendelee; https://youtu.be/ewEhyU0Q3hc

SIMU.TV: Rais Dkt John Magufuli leo amepokea hati sita za utambulisho wa mabalozi kutoka nchi mbalimbali wanaokuja nchini kuziwakilisha nchi zao; https://youtu.be/a6bNdVgG4_k

SIMU.TV: Mkuu wa mkoa wa Kigoma Emmanuel Maganga amesema serikali mkoani humo itawalinda raia wema wanaowafichua wahamiaji haramu; https://youtu.be/ti0LjAq9GHg

SIMU.TV: Kamati ya kudumu ya bunge ya uwekezaji wa mitaji ya umma imeishauri serikali kuweka mitaji ya kutosha katika taasisi za umma; https://youtu.be/cpW2nN2MGiM

SIMU.TV: Shirika la nyumba NHC limezindua ujenzi wa nyumba 300 za watumishi wa serikali kwa lengo kusaidia mchakato wa kuhamia Dodoma; https://youtu.be/9pQGsXaclhw

SIMU.TV: Uwezo wa shilingi 100 ya kitanzania kununua bidhaa mbalimbali umeporomoka zaidi kutokana na kuongezeka failisi za bei ya Taifa; https://youtu.be/QzHemShLzBA

SIMU.TV: Jahazi la timu ya JKT Ruvu limezidi kuzama baada ya leo kukubali kipigo cha goli moja kwa  bila kutoka kwa Tanzania Prisons; https://youtu.be/NOcR2LNOpuM

SIMU.TV: Jukwaa la maonyesho ya mitindo na ubunifu wa mavazi maarufu kama Lady in Red linatarajia kufanyika nchini huku wadau wa mitindo wakiombwa kujitokeza; https://youtu.be/YalubSdbLcU

SIMU.TV: Timu ya JKT Oljoro imezidi kufufua matumaini ya kurejea tena ligi kuu Tanzania bara baada ya kufanya vizuri kwenye ligi daraja la pili; https://youtu.be/utVLc7byU_A

SIMU.TV: Nahodha wa zamani wa timu ya Taifa ya Ujerumani Philip Lahm amedokeza kuwa mwishoni mwa  msimu huu atastaafu kucheza soka; https://youtu.be/zIaqKZjC8UU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...