JESHI LA ULINZI
LA WANANCHI WA TANZANIA
KURUGENZI YA
HABARI NA UHUSIANO
Simu ya Upepo : “N G O M E”
Makao Makuu ya Jeshi,
Simu ya Mdomo:
DSM 22150463 Sanduku la Posta 9203,
Telex
: 41051 DAR ES SALAAM, 31 Januari, 2017.
Tele Fax
: 2153426
Barua
pepe : ulinzimagazine@yahoo.co.uk
Tovuti : www.tpdf.mil.tz
Jeshi la
Ulinzi la Wananchi wa Tanzania limesikitishwa na taarifa iliyotolewa na gazeti
la Tanzania Daima toleo Nambari 4438 la tarehe 28 Januari 2017, Habari
leo la tarehe 29 Januari 2017 na baadhi ya
vyombo vya habari vikihusisha mauaji ya kondakta wa daladala na Wanajeshi
Mkoani Tanga.
Tunapenda kuwataarifu wananchi kwamba kwa mujibu wa
jeshi la polisi watuhumiwa wanaoshikiliwa na Jeshi hilo ni wanne (4),mmoja kati
yao ni Mwanajeshi ambaye ni mzazi wa msichana anayetuhumiwa kusababisha tukio
hilo.
Hivyo Mwanajeshi huyo anashikiliwa kwa ajili ya kulisaidia Jeshi la
Polisi katika uchunguzi kwa kuwa tukio hilo lilifanyika nyumbani kwake. Hakuna
Wanajeshi waliohusika katika tukio hilo kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo
vya habari, kambi za Jeshi wanaishi Wanajeshi pamoja na familia zao hivyo
kuhusisha moja kwa moja mauaji hayo na Wanajeshi mkoani Tanga ni kuupotosha umma.
Wito
unatolewa kwa vyombo vya habari kuripoti habari zenye ukweli.Habari zisizo za
kweli zinapotosha umma na kujenga taswira potofu kwa wananchi dhidi ya Jeshi la
Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari
na Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P 9203, Dar es Salaam, Tanzania.
Kwa Mawasiliano zaidi: 0756-716085
ni aibu jeshi kutumia yahoo account kwenye official email. Siri za jeshi zinaweza kuvuja kirahi , nawaomba tafadhali badilisha haraka.
ReplyDelete