JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA NISHATI NA MADINI


  
TAARIFA KWA UMMA

AWAMU YA KWANZA YA WATUMISHI KUHAMIA MAKAO MAKUU YA NCHI - DODOMA TAREHE 10 FEBRUARI, 2017

Wizara ya Nishati na Madini inapenda kuufahamisha umma kuwa, Awamu ya Kwanza ya Watumishi wa Wizara kuhamia Makao- Makuu ya Nchi, Dodoma inaanza tarehe 10 Februari, 2017.

Miongoni mwa watakao hamia katika awamu hiyo ni pamoja na Viongozi na Watendaji Wakuu wa Wizara ambao ni Waziri wa Nishati na Madini, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na Naibu Makatibu Wakuu wa Nishati na Madini.

Watumishi wengine ni pamoja na Kamishna wa Madini Tanzania, Kamishna wa Nishati na Masuala ya Petroli, Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala na Maafisa. Jumla ya Watumishi wanaohamia Dodoma Awamu ya Kwanza ni 47.

Aidha, kutokana na uhamisho huo, anuani ya Wizara  Dodoma ni;
Katibu Mkuu,
Wizara ya Nishati na Madini,
Barabara ya Kikuyu,
S.L.P 422,
DODOMA
Imetolewa na;

KATIBU MKUU
WIZARA YA NISHATI NA MADINI
9/2/2017


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...