Wafanyabiashara kuunganishwa na huduma mpya ya intanenti ya  gharama nafuu ya kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania ili kuwarahisishia mawasiliano katika biashara zao ambapo gharama ya kuunganishwa zinawezesha unafuu wa shilingi 330,000/-

Huduma hii iliyolenga kuwarahishia mawasiliano wafanyabiashara pia inawawezesha kufurahia huduma ya internet yenye kasi kubwa kutoka mtandao wa Vodacom.
Huduma hii ya aina yake nchini inawezesha mteja kujipatia Kbs256  kwa gharama ya shilingi 100,000/-kwa mwezi ikiwemo na kodi ya ongezeko la thamani ambapo pia wanaweza kujipatia Mbps 2 kwa mwezi kwa gharama ya shilingi 200,000/- na huduma hizi zote mbili zinawawezesha kutumia internet bila kikomo. 
Wateja wataunganishwa na huduma hii kutokana na mahitaji yao na watafungiwa vifaa vya kisasa vya uwezeshaji wa internet kwa kadri ya  watumiaji watakaotumia huduma hii kwenye biashara au taasisi.
Kwa watakaohitaji huduma hii wakaingia mkataba maalumu na kampuni ya Vodacom ambao utadumu kwa kipindi cha miaka 2”.Alisema Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Jacquiline Materu.
Alisema kuwa kampuni yao imekuja na huduma hii maalumu kwa kuwa wakati wote inaleta ubunifu wa huduma zinazoendana na mahitaji ya wateja wake lengo kubwa likiwa ni kuwapatia huduma za uhakika za mawasiliano na za gharama nafuu ili kuwarahisishia maisha na kuwawezesha kufurahia intanenti yenye kasi kubwa nchini kutoka Vodacom. 
Kupata huduma hii anachotakiwa kufanya mteja ni kutuma maombi kwenye barua pepe ya vodacombiashara@Vodacom.co.tz.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...