Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Ubalozi wa Kuwait nchini umekabidhi visima vinne katika shule za msingi Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Shule za Msingi  zilizopata visima hivyo ni Yombo, Umoja , Mwale pamoja na Bwawani. Akizungumza  wakati wa kukabidhi visima hivyo, Balozi wa Kuwait , Jasem Al-Najem  amesema kuwa wanatambua umuhimu wa maji ndiyo maana wameona umuhimu wa visima hivyo katika shule hizo.

Amesema wataendelea kutoa misaada hiyo kutokana na mahitaji yaliyopo katika jamii kutokana na ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Kuwait.

Al-Najem amesema kuwa wameweza kuchimba visima 16 vyenye thamani ya  Dola za Kimarekani 63,000  na watu wengine waweze kujitokeza kusaidia jitihada mbalimbali.

Ubalozi huo pia umekabidhi dawa za binadamu katika Hospitali ya Amana zenye thamani  sh.milioni tatu.
Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem akizundua kisima cha maji safi katika shule ya Msingi Yombo jijini Dar es Salaam, Kulia ni Naibu Mkurugenzi wa Red Cresene , Anwari Abdallah Al-Hasawi.Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.
Afisa Elimu, Elimu ya Watu Wazima wa Manispaa ya Ilala , Hamisi Mlangala akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa visima ambapo alishukuru msaada huo.
Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem akikabidhi dawa kwa Mganga Mkuu Msaidizi wa Hospitali ya Amana, Amimu Kilomoni, jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Kuwait nchini , Jasem Al-Najem akitembelea Wodi ya Watoto katika Hospitali ya Amana  jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...