Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Benki ya CRDB imedhamiria kuwainua wanawake kiuchumi kwa kuwawezesha kwa kufungua akaunti ya Malkia ambayo itakuwa ni yenye malengo yakinifu na manufaa kwa maendeleo kwa wanawake.

Akizungumza na Globu hii, Muhamasishaji wa kampeni katika wiki ya wanawake kutoka benki ya CRDB Mary Gekura, amesema kuwa akaunti hii ya Malkia inakuwa na malengo makuu ya kumuwezesha mwanamke ili aweze kuwa na malengo yakinifu ya kujiendeleza kiuchumi.

Mary amesema kuwa, kampeni hii imeanza machi mosi na itakuwa ni endelevu na taratibu zake za kufungua ni kwa kima cha chini cha shilingi cha elfu hamsini (50,000) na mteja atatakiwa kuweka hela kwa muda wa mwaka mmoja bila kuzitoa.

Amefafanua kuwa, ndani ya mwaka mmoja mteja anaweza kupata faida ya kutosha na kuanzisha miradi mbalimbali.
 Mkurugenzi wa tawi la CRDB Water Front Donath Shirima (kulia) akiwa pamoja katika picha na wafanyakazi wa tawi hilo kuelekea maadhimisho ya wiki ya wanawake duniani  Machi 08 mwaka huu.
 Wafanyakazi wa wa tawi la CRDB Water Front katika picha za pamoja kuelekea maadhimisho ya wiki ya wanawake duniani Machi 08 mwaka huu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...