Katibu wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Stanley Mkandawile akizungumza na baadhi ya viongozi wa Jumuia hiyo kutoka katika Kata mbalimbali za wilaya ya Ilala, alipokutana nao katika kikao maalum cha kujitambulisha kwao, kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Ilala. Kulia ni Katibu wa Jumuia hiyo wilaya ya Ilala, Lugano Mwafongo. 

Akizungumza kwenye kikao hicho, pamoja na mambo mbalimbali Mkandawile ameitaka Jumuia ya Wazazi katika mkoa wake na maeneo mengine nchini, kuunga mkono hatua ya serikali kuingia katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya.

Mkandawile amesema, Kama sehemu ya Wanana CCM, Jumuia hiyo haiba budi kuunga mkono mabambano hayo kwa kuwa Serikali inatekeleza ilani ya CCM, ibaraya 118 hadi 119.
Katibu wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Stanley Mkandawile akiwasili ukumbini. Kushoto ni Katibu wa Jumuia hiyo wilaya ya Ilala, Lugano Mwafongo na kulia ni Katibu wa Jimbo la Ilala Christopher Lugemalila.
Wajumbe wakimsikiliza Mkandawile wakati akizungumza na watendaji na viongozi wa Jumuia ya Wazazi Wilaya ya Ilala. Picha zote na Bashir Nkoromo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...