Bila shaka kila mmoja wetu anakumbuka ahadi ya RC Makonda aliyoitoa mwaka jana ya kujenga viwanja vitatu (3) vya mpira kwa ajili ya maendeleo ya mashindano mbalimbali ya michezo ikiwemo Ndondo Cup kwani mashindano haya kwa ujumla wake yanalenga kuboresha mazingira ya michezo na kuzalisha vipaji vingi zaidi ambavyo vinabeba ajira nyingi za vijana ndani yake.

Kimsingi RC Makonda hakuishia tu kuahidi bali alikwenda mbali zaidi na kumualika balozi wa China kushuhudia hali halisi ya viwanja vinavyotumika kwa sasa kama sehemu ushahidi wa kile alichokuwa amemueleza wakati akimshawishi.

Ikiwa imepita miezi kadhaa tangu Balozi kukubaliana na ombi la Mkuu wa Mkoa, leo tarehe 3 Balozi huyo wa China akiwa na RC Makonda wameweka historia mpya baada ya kuweka jiwe la msingi la kuanza ujenzi wa viwanja hivyo, huku wakianza na kiwanja cha Bandari ambacho kitagharimu Dola za Kimarekani 450,000,

Huku kikijengwa kwa viwango vya kimataifa na kampuni iliyojenga uwanja wetu wa taifa. Kuonyesha na kutambua utendaji na msukumo mkubwa wa RC Makonda katika kutimiza azma ya Rais John Pombe Magufuli ya kutatua changamoto za wanyonge, Balozi pia amemuahidi Mkuu wa Mkoa kutoa kipaumbele cha ajira vijana wote watakaoshiriki mashindano ya Ndondo Cup kwenye kampuni mbili ambao watakuwa vijana zaidi ya 20000.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda kwa kushirikiana na Balozi wa China nchini Tanzania Dkt. Lu Youqing wakiweka jiwe la msingi kuanza ujenzi wa kiwanja cha Bandari ambacho kitagharimu Dola za Kimarekani 450,000,jana jijni Dar e Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akiteta jambo na Balozi wa China nchini Tanzania Dkt. Lu Youqing jana jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akizungumza katikahafla ya uwekaji wa jiwe la msingi kuanza ujenzi wa kiwanja cha Bandari ambacho kitagharimu Dola za Kimarekani 450,000, jana jijni Dar e Salaam.
Balozi wa China nchini Tanzania Dkt. Lu Youqing akizungumza katika hafla yauwekaji wa jiwe msingi kuanza ujenzi wa kiwanja cha Bandari ambacho kitagharimu Dola za Kimarekani 450,000, jana jijni Dar e Salaam.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hongera sana RC Makonda ,ila naomba niumbusje umuhimu wa wadau wa michezo kukumbuka kuwa Football sio mchezo pekee unaoweza kulinyanyua Taifa ,Ni vyema kuangalia miundombinu ya michezo mingine pia kama Tennes ,Volleyball ,Badminton ,Basketball na mengineyo mingi...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...