Na chalila Kibuda,Globu ya jamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira, January Makamba amesema shehena za viroba vilivyopatikana katika viwanda,Maghala, Maduka ya Usambazaji pamoja na sehemu za starehe zikae kizuizini mpaka serikali itakapotoa tamko kwa watu hao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo wakati akitoa taarifa ya operesheni, Makamba amesema viroba vilivyokamatwa vina thamani ya sh. bilioni 10.83 na operesheni inaendelea kwa kuwahusisha wenyeviti wa serikali za mitaa.

Amesema kuwa operesheni hiyo imebaini kuwepo viroba vyenye Stika za Mamlaka Mapato Nchini (TRA) zikiwa zimegushiwa na wanaofanya biashara hiyo.Makamba amesema watu waliofanya ukiukaji wa Sheria wa biashara hiyo wanajiandaa kuwafungulia mashitaka.

Waziri Makamba amesema na viroba vilivyopatikana baadhi watavipeleka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali juu ya madhara kwa matumizi ya binadamu.
Aidha amesema kuna baadhi wafanyabiashara walikwenda kufungua kesi ya kuzuia operesheni waligonga mwamba kutokana sheria ya kufanya kazi hiyo.

Aliongeza kuwa kuna baadhi raia wa kigeni wanafanya kazi bila kibari na kutaka Idara ya Uhamiaji kufatilia raia hao.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, January Makamba akizungumza na waandishi habari juu matokeo ya operesheni viroba leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...