Mkurugenzi
Mtendaji waShirika la Misaada ya Maendeleo la Uingereza DFID katika
Benki ya Dunia Bw.David Kinder amepongeza hatua iliyofikiwa na serikali
ya Tanzania kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF- katika kuteleza
Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini,PSSN.
Bw. Kinder ametoa pongezi hizo baada ya kukutana na walengwa wa Mpango huo katika vijiji vya Mzenga A na Vilabwa katika wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani ambako amejionea mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta za uboreshwaji wa makazi,elimu,lishe na afya kwa walengwa hao.
Amesema hatua iliyofikiwa na walengwa hao inapaswa kuungwa mkono zaidi ili hatimaye waweze kuondokana na madhira ya umasikini unaowakabili.
Kwa upande wao, baadhi ya walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika vijiji hivyo wamesema tangu kuanza utekelezaji wa Mpango huo wameanza kuona fursa za maendeleo ikiwemo kuezeka mabati nyumba zao, kufuga kuku, na hata kuongeza shughuli za kilimo.

Bi.Asha Khalifan Kikombe mmoja wa Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaotelezwa na TASAF katika kijiji cha Vilabwa ,Wilaya ya Kisarawe ,mkoani Pwani akiwaonyesha wageni kutoka Shirika la Misaada la Uingereza (hawako pichani) nyumba aliyoezeka kwa mabati alizozinunua kwa kutumia fedha za ruzuku kutoka TASAF
Ujumbe kutoka DFID wakiwa na baadhi ya watendaji kutoka TASAF na Halmashauri ya wilaya ya Kisarawe wakipata maelezo ya mradi wa kutunza mazingira unaotekelezwa na walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini kwa utaratibu wa Ajira ya Muda unaotekelezwa wakati wa kipindi cha hari kwa lengo la kuwaongezea walengwa kipato.
Baadhi ya walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Msikini katika kijiji cha Mzenga A wilaya ya Kisarawe wakishiriki katika mkutano ulioitishwa kuzungumzia mafanikio ya utekelezaji wa shughuli za Mpango uliohudhuriwa pia na wageni kutoka Shirika la Misaada la Uingereza DFID.
Ujumbe kutoka Shirika la Misaada la Uingereza DFID ukipata maelezo kutoka kwa mmoja wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Vilabwa juu ya namna alivyonufaika na fedha zinazotolewa na serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jmii TASAF.
Ujumbe kutoka Shirika la Misaada la Uingereza DFID ukipata maelezo kutoka kwa mmoja wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Vilabwa juu ya namna alivyonufaika na fedha zinazotolewa na serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jmii TASAF.
Bw. Kinder ametoa pongezi hizo baada ya kukutana na walengwa wa Mpango huo katika vijiji vya Mzenga A na Vilabwa katika wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani ambako amejionea mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta za uboreshwaji wa makazi,elimu,lishe na afya kwa walengwa hao.
Amesema hatua iliyofikiwa na walengwa hao inapaswa kuungwa mkono zaidi ili hatimaye waweze kuondokana na madhira ya umasikini unaowakabili.
Kwa upande wao, baadhi ya walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika vijiji hivyo wamesema tangu kuanza utekelezaji wa Mpango huo wameanza kuona fursa za maendeleo ikiwemo kuezeka mabati nyumba zao, kufuga kuku, na hata kuongeza shughuli za kilimo.

Bi.Asha Khalifan Kikombe mmoja wa Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaotelezwa na TASAF katika kijiji cha Vilabwa ,Wilaya ya Kisarawe ,mkoani Pwani akiwaonyesha wageni kutoka Shirika la Misaada la Uingereza (hawako pichani) nyumba aliyoezeka kwa mabati alizozinunua kwa kutumia fedha za ruzuku kutoka TASAF

Ujumbe kutoka DFID wakiwa na baadhi ya watendaji kutoka TASAF na Halmashauri ya wilaya ya Kisarawe wakipata maelezo ya mradi wa kutunza mazingira unaotekelezwa na walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini kwa utaratibu wa Ajira ya Muda unaotekelezwa wakati wa kipindi cha hari kwa lengo la kuwaongezea walengwa kipato.

Baadhi ya walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Msikini katika kijiji cha Mzenga A wilaya ya Kisarawe wakishiriki katika mkutano ulioitishwa kuzungumzia mafanikio ya utekelezaji wa shughuli za Mpango uliohudhuriwa pia na wageni kutoka Shirika la Misaada la Uingereza DFID.

Ujumbe kutoka Shirika la Misaada la Uingereza DFID ukipata maelezo kutoka kwa mmoja wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Vilabwa juu ya namna alivyonufaika na fedha zinazotolewa na serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jmii TASAF.

Ujumbe kutoka Shirika la Misaada la Uingereza DFID ukipata maelezo kutoka kwa mmoja wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika kijiji cha Vilabwa juu ya namna alivyonufaika na fedha zinazotolewa na serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jmii TASAF.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...