Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akijibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa mara baada ya kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18 katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa wakipitia kwa makini taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18 ya Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora iliyowasilishwa na Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...