Na Freddy Macha
Jumuiya ya
Wasanii wa Tanzania Uingereza (WASATU) leo inazinduka kwa onesho la muziki
Northampton.
Onesho hilo litajumuisha wanamuziki wakongwe wa Kitanzania wakiwemo Saidi Kanda
( na bendi Mvula Mandondo), mwimbaji sauti chiriku Fab Moses na bendi ya Afrika
Jambo ikihusisha mpiga sax RamaSax. Ramasax aliwahi kupuliza “madude” na Simba
wa Nyika. Mwingine ni mpiga gitaa Kawele Mutimanwa aliyeshiriki wimbo maarufu
wa Mambo Bado na bendi ya Makassy miaka ya 80. Wengine ni pia wanamuziki
walemavu kama mpiga gitaa John Londo, Kea nk...
Mwenyekiti wa
WASATU, Bi Neema Kitilya , mcheza dansi, Khadija ( Kibisa zamani) wasanii
wengine wameeelezea mori wao kutangaza na kujumuiha wasanii wetu duniani.
TUTAWALETEA HABARI ZAIDI INSHALLAH MUNGU AKIPENDA
Tuko pamoja!
Tanzania
oyeee !!!
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...