
Mbunge wa Singida Mjini, Mheshimiwa Mussa Sima amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa SIREFA baada ya kuwashinda wenzake Erasto Sima, Hussein Mwamba, Said Mnyampanda na Samwel Nakei.
Katika salamu zake kwa SIREFA, Rais Malinzi amesema anashukuru kwa uamuzi wa kidemokrasia uliofanywa na wajumbe wa mkoa huo na kwamba ana imani na uongozi ulioingia madarakani.
“Kwa namna ya wanafamilia wa mpira wa miguu wa Mkoa wa Singida walivyodhamiria kutaka kuleta maendeleo ya mpira wa miguu, nina imani na uongozi wa Mheshimiwa Sima katika kutekeleza mipango ya maendeleo ya soka mkoani huo,” amesema Malinzi.
Katika uchaguzi huo mdogo uliofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) mjini Singida na kusimamiwa na Mwenyekiti Stella Maila, pia ulimchagua Katibu Mkuu Rashid Koba wakati Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF ni Nurfus Ndee huku Hamza Ntoga akichaguliwa kuwa Mweka Hazina Msaidizi.
Nafasi ya Makamu Mwenyekiti ilikwenda kwa Ally Ramadhani Nkhangaa aliyekuwa mgombea pekee wakati Koba alimshinda Edward Ihonde na Ndee alimshinda Manase Abel.
Uchaguzi wa SIREFA ulifanyika baada ya viongozi wengine walioingia madarakani mwishoni mwa mwaka jana, kujiuzulu kutokana na kubanwa na majukumu mbalimbali.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...