Mkuu wa mkoa Mhe. Mrisho Gambo mapema leo amezindua mradi mkubwa wa
maji wa maji kwaajili ya kunyweshea mifugo(cattle trough) na matumizi
ya binadamu katika kata ya Ndepes wilayani Ngorongoro.
Mradi
huo mkubwa wa maji umetumia takribani milioni 200 ikiwa ni gharama nzima
za mradi huo, utekelezaji wa mradi huo umesimamiwa na mamlaka ya
hifadhi ya Ngorongoro ikiwa ni utekelezaji wa agizo la waziri mkuu Mhe.
Kassim Majaliwa alilolitoa mapema mwezi wa Desemba 2016, moja ya maagizo
yake ilikua ni wananchi kujengewa mfumo wa maji kwa matumizi yao na
mifugo yao ili kuzuia uingizwaji wa mifugo katika crater ya Ngorongoro.
Aidha
Mhe. Gambo ameipongeza mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro kwa kuutekeleza
mradi huo kwa wakati na kuendelea kutoa msisitizo kwa wananchi kuwa
agizo la kutoingiza mifugo ndani ya crater linaendelea na amezitaka
mamlaka kuanza mchakato wa kuligeuza agizo hilo kuwa sheria ili liweze
kutekelezeka kwa vitendo zaidi.
Wananchi wa eneo la Ndepes
wameishukuru sana serikali ya awamu ya tano kwa kutekeleza ahadi yake ya
kuhakikisha wananchi hawafuati maji umbali zaidi ya mita mia nne kama
ilivyo ahidiwa katika ilani ya Chama Cha Mapinduzi.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...