KAMPUNI ya Mitindo ya BlackFox Models inazidi kujitanua huku ikiwatengenezea fursa vijana kukuza vipaji vyao mbalimbali.
Hivi
karibuni Kampuni hiyo ilifanya usahili wa wanamitindo mkoani Mwanza
ambapo mamia ya vijana walijitokeza na kunolewa huku wakijipatia
mikataba ya kufanya kazi na kampuni hiyo.
Lakini pia imewachukua washiriki wa Miss Ardhi University ambao walishika nafasi tatu bora katika shindano hilo.
Washiriki hao ni Glady John, Stella Ernest na Evodia Patrick.
Akizungumzia
maendeleo ya kampuni hiyo Mkurugenzi Mtendaji wake, Atu Mynah, Aj
alisema kuwa lengo kubwa ni kuwajengea uwezo vijana wakitanzania.
Alisema,
amehakikisha kuwa anawasaka vijana wenye nia ya kuwa wanamitindo na
kuwaendeleza hadi kufikia malengo yao huku akisisitiza kuwa anawanoa
katika misingi yote ya uanamitindo.
Alisema, anawaendeleza
katika vipaji vyao ikiwa ni sambamba na kuwapatia elimu ya fani hiyo
kuanzia kibiashara, kisheria na kila kinachotakiwa kwa mtu kuwa
Mwanamitindo.
AJ, kushoto akipitia profile za baadhi ya wanamitindo walioomba kushiriki kwenye usahili huo.
Meza ya majaji ikiendelea na mchakato wa kuwapata wanamitindo.
Aj, akizungumza na wanamitindo kadhaa waliofanikiwa kuchaguliwa ambapo alisikika akisisitiza suala zima la nidhamu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...