Suleiman Msuya
IKIWA ni takribani miezi
10 sasa kwa Chama cha Wananchi (CUF), upande wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif
Hamad kuvamiwa katika Ofisi Kuu za Bugurunina kundi la Profesa Ibrahim
Lipumba chama hicho kimezindua ofisi mpya za chama hicho katika eneo la Mtaa wa Idrisa,
Kata ya Mzimuni, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Aidha,
Seif amesisitiza kuwa hatarajii kukutana na Profesa Lipumba kwa kile
alichodai kuwa hatambuliki katika chama na hana sifa hizo kwa sasa.
Akizindua ofisi hiyo ambayo lengo kubwa ni kwa ajili ya wabunge
40 wa CUF, Seif alisema uamuzi wa wabunge hao kumpatia ofisi ya kufanyia kazi hapo ni cha
kiungwana na kinahitajika kuungwa mkono na wanachama wote.
Alisema kwa muda wa miezi
10 sasa wamekuwa wakishindwa kufanya kazi hasa upande wa Tanzania Bara
jambo ambalo limewaathiri sana hivyo kupatiwa ofisi kutamsaidia kutimiza majukumu yake vilivyo bila hofu yoyote.
Maalim Seif alisema kukosa ofisi kumewaathiri sana katika baadhi ya
mambo hivyo anaamini kwa sasa akifikia Dar es Salaam anamahali pa
kukutana na wakurugenzi wake.
“Nimekuwa ni kija hapa nakosa sehemu ya kukutana na wakurugenzi,
viongozi mbalimbali wanachama ila hiki ambacho wabunge wamefanya ni cha
kuungwa mkono sijawahi kufanya kazi na wabunge wanao kipenda chama kama kipindi hiki,”
alisema.
Katibu huyo alisema atahakikisha kuwa anaanza kazi haraka iwezekanavyo kwa kukutana na wakurugenzi
wake ili waweze kutekeleza majukumu ya chama.
“Hakuna
shaka kuwa hu u unaoitwa mgogoro umeturudisha nyuma sana hivyo naamini
wakati wa kufanyakazi umerejea na hawa wabaya wetu hawata ambulia kitu
kwani
CUF ni chama imara hakitikisiki,” alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...