Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
MAMLAKA wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA)imejizatiti kwa kufanya marekebisho ya sheria ikiwa ni katika kuboresha zaidi manunuzi ya bidhaa na vifaa kwa serikali.
Akizungumza wakati akitembelea banda la PPRA lililopo kwenye jengo la Wizara ya Fedha na Mipango, Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA Dkt Laurent Shirima amesema kuwa maboresho hayo yatalenga katika sehemu tano ambazo zitaboresha manunuzi ya zabuni katika nyanja mbalimbali.
Dkt Shirima amesema kuwa sheria hiyo imeboreshwa katika kupunguza gharama za ununuaji wa Bidhaa na vifaa, serikali kununua kwa bei za sokoni wakimaanisha bei halisi ya bidhaa na vifaa pia wametoa upendeleo kwa makampuni ya ndani ikiwemo makundi maalumu kama vile wanawake, wazee na vijana.
Ameongezea kuwa, katika maboresho mengine yaliyofanywa ni katika kuendeleza viwanda kama serikali ya awamu ya tano inavyosisitiza ukuaji wa viwanda huku PPRA ikiangalia zaidi wataalamu wa manunuzi kutoka ndani pia wapo katika hatua za mwisho za kuhamia katika mfumo wa kieletroniki wa ununuzi wa zabuni.
PPRA ni mamlaka inayohusiana na udhibiti wa manunuzi ya Umma ambapo kupitia kwa Mtendaji Mkuu Dkt Shirima amewaondoa hofu wananchi kuwa waiamini taasisi yao kwani mambo mengi ya msingi yameshawekwa wazi na fedha za umma zinahitaji uwajibikaji.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma PPRA Dkt Laurent Shirima akizungumza na wanahabari wakati alipotembelea banda la Mamlaka wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma PPRA lililopo kwenye jengo la Wizara ya Fedha na Mipango na kuelezea namna wanavyojizatiti katika kuboresha ununuaji wa zabuni kwa serikali.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) Dkt Laurent Shirima akimuhudumia mwananchi aliyetembelea banda lao na katika maadhimisho ya 41 ya Monesho ya kimataifa ya Sabasaba leo Jijini Dar es salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka wa Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) Dkt Laurent Shirima akipata maelezo kutoka kwa mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa Taifa (PPF) wakati alipotembelea banda hilo lilipo katika Jengo la Wizara ya Fedha na Mipango katika maadhimisho ya 41 ya Monesho ya kimataifa ya Sabasaba leo Jijini Dar es salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...