Na,Jumbe Ismailly SINGIDA July,03,2017 Nyalandu 


MBUNGE wa Jimbo la Singida Kaskazini,Lazaro Nyalandu ametangaza donge nono kwa timu itakayokuwa bingwa wa mashindano ya kombe la Mbunge huyo,maarufu kwa jina la “NYALANDU CUP” linalotarajia kuanza mwezi wa nane mwaka huu.

Kombe hilo litakaloanza mwezi ujao,litashirikisha timu za mpira wa miguu kwa wanaume na mpira wa miguu kwa wanawake na kilele cha mashindano ya kombe hilo kitafanyika katika Kijiji cha Ngamu,kilichopo katika Kata ya Mwasauya.

Akitangaza msimamo wake huo mbele ya Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2017,Amour Hamad Amour,Nyalandu alisema kwamba tangu alipochaguliwa kuwa mwakilisha wa wananchi wa jimbo hilo la Singida Kaskazini hajawahi kuandaa ligi ya aina yake kama hiyo inayotarajiwa kuanza kuchezwa katika jimbo zima.

“Nilimwambia Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru nafikiri nilikuwa namnong’oneza kwamba mwenge ukipita na hii itakuwa ni mara ya kwanza tangu nimekuwa Mbunge halafu kuchezesha mambo hii ya mechi”alifafanua ‘Mimi nafanyaaga maskolashipu,wasome sekondari,wafanye nini,mambo ya maji nafikiri sasa hivi tutaenda kwa zote, kwa hiyo ningependa kuanzisha ligi ambayo itafanyika ya mpira wa miguu lakini nataka iende sambamba na ligi ya wanawake” alisisitiza Mbunge Nyalandu.

Kwa mujibu wa Mbunge huyo kutakuwa na ligi ya wanaume na itafungwa pamoja na ligi ambayo itakuwa ni ya wanawake na ligi hiyo watashirikiana kuitangaza,kuiunda na kuiandaa na serikali ya wilaya hiyo pamoja na Halmashauri hiyo kwa ujumla.
Mchezaji wa timu ya Mtinko Fc,Yusufu Samsoni (mwenye jesi yenye rangi ya bluu) alipomtoka mchezaji wa timu ya Msange Fc,Yasini Athumani na kwenda kuifungia timu yake bao la pili na la ushindi.
Baadhi ya wachezaji wa timu ya Msange FC wakifanya mazoezi katika uwanja wa michezo wa shule ya msingi Mtinko kabla ya kuanza kwa mchezo huo ambao matokeo yalikuwa Mtinko FC 2 na Msange FC 1.(Picha zote Na Jumbe Ismailly).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...