Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) Dkt. Zainab Chaula (wa pili kushoto) akipokea sehemu ya
msaada wa vifaa tiba, kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa
PPF, William Erio kwa ajili ya Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, katika
hafla fupi ya makabidhiano hayo iliyofanyika Hospitalini hapo, Julai 22,
2017. Wengine pichani ni Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Rehema Madenge
(katikati), Mjumbe wa Bodi ya Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Sarah Mwaga
(wa pili kulia) pamoja na Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dkt.
Caroline Damian. Mfuko huo umetoa msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya
shilingi milioni 99 kwa hospitali 16 hapa nchini ikiwa ni sehemu ya
kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha sekta ya afya.
Naibu
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) Dkt. Zainab Chaula (wa nne kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa
Mfuko wa Pensheni wa
PPF, William Erio (katikati) wakiangalia moja ya vitanda vya
kujifungulia wakina mama, vilivyotolewa na Mfuko huo, kwa Hospitali ya
Mkoa wa Dodoma, Julai 22, 2017.
Katibu
Tawala Mkoa wa Dodoma, Rehema Madenge akizungumza kabla ya kumkaribisha
mgeni rasmi, katika hafla fupi ya makabidhiano msaada wa vifaa tiba
vilivyotolewa na
Mfuko wa Pensheni wa PPF kwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Julai 22,
2017.
Mkurugenzi
Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio akizungumza katika hafla
fupi ya makabidhiano msaada wa vifaa tiba vilivyotolewa na Mfuko wa
Pensheni wa PPF kwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Julai 22, 2017.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...