BENKI ya NMB leo imekabidhi vifaa vya michezo kwa timu ya Jeshi la
Wananchi Tanzania (JWTZ) inayotarajia kushiriki Mashindano ya Kijeshi ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki itakayofanyika jijini Bujumbura - Burundi.
Vifaa vilivyokabidhiwa leo ni pamoja na mipira kwaajili ya timu ya mpira
wa miguu, mipira ya mchezo wa mikono (wasichana) na mipira mchezo wa
kikapu kwa wanaume (Basket ball).
Akikabidhi
vifaa hivyo kwa Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa JWTZ -
Kanali Richard Mwandike, Kaimu Afisa Mkuu wa Wateja wadogo na Wakati wa
NMB - Boma Raballa alisema vifaa vingine ni pamoja na mipira 10 ya
mchezo wa volebo (Volleyball), jezi 42 za mpira wa miguu, seti mbili za
jezi mpira wa kikapu (wasichana), seti mbili za jezi mpira wa basket na
seti mbili za jezi mpira wa Volleyball.
Vifaa
vingine vilivyokabidhiwa ni pamoja na seti mbili za jezi za waamuzi kwa
michezo ya Netball, Basketball, Volleyball na mabegi 30 ya wachezaji
ambapo vyote kwa ujumla vina thamani ya shilingi milioni 10 za
Kitanzania.
Bw. Raballa alisema kuwa msaada huo umetokana na ushirikiano mzuri na wa
muda mrefu kati ya benki ya NMB na jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) na
ndiyo maana wakaona umuhimu wa kuendelea kuwashika Mkono kupitia msaada
kwa timu za jeshi zinazoenda kushiriki mashindano ya majeshi ya jumuia
ya afrika ya mashariki.
"...Hii
si mara ya kwanza kusaidia katika mashindano haya, kwani nakumbuka hata
mwaka jana tuliwasaidia baadhi ya vifaa vya michezo kushiriki katika
mashindano haya. Tunaamini vifaa hivi mbali na kuendeleza ushirikiano
wetu mzuri, vitakuwa chachu ya kufanya vizuri katika mashindano haya
muhimu kwa jumuia ya Afrika ya Mashariki," alisema Raballa.
Kaimu Afisa Mkuu wa Wateja wadogo na Wakati wa NMB - Boma Raballa (kushoto) akimkabidhi vifaa mbalimbali vya michezo Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) - Kanali Richard Mwandike (kulia) leo jijini Dar es Salaam.
Vifaa hivyo mbalimbali vya michezo zikiwemo jezi, mipira na vifaa vingine vyenye thamani ya shilingi milioni 10, vitatumiwa na wachezaji wa timu ya JWTZ wanaotarajia kusjiriki Mashindano ya Kijeshi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayotarajia kuanza Agosti 24, 2017.Kaimu Afisa Mkuu wa Wateja wadogo na Wakati wa NMB - Boma Raballa (kushoto) akimkabidhi vifaa mbalimbali vya michezo Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) - Kanali Richard Mwandike (kulia) leo jijini Dar es Salaam. Vifaa hivyo mbalimbali vya michezo zikiwemo jezi, mipira na vifaa vingine vyenye thamani ya shilingi milioni 10, vitatumiwa na wachezaji wa timu ya JWTZ wanaotarajia kusjiriki Mashindano ya Kijeshi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayotarajia kuanza Agosti 24, 2017.Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) - Kanali Richard Mwandike (kulia) akimshukuru Kaimu Afisa Mkuu wa Wateja wadogo na Wakati wa NMB - Boma Raballa (kushoto) mara baada ya kupokea vifaa mbalimbali vya michezo leo jijini Dar es Salaam vilivyotolewa na NMB kuwezesha timu ya JWTZ kushiriki Mashindano ya Kijeshi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayotarajia kuanza Agosti 24, 2017.Kaimu Afisa Mkuu wa Wateja wadogo na Wakati wa NMB - Boma Raballa (kushoto) akimkabidhi vifaa mbalimbali vya michezo Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) - Kanali Richard Mwandike (kulia) leo jijini Dar es Salaam. Vifaa hivyo mbalimbali vya michezo zikiwemo jezi, mipira na vifaa vingine vyenye thamani ya shilingi milioni 10, vitatumiwa na wachezaji wa timu ya JWTZ wanaotarajia kusjiriki Mashindano ya Kijeshi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayotarajia kuanza Agosti 24, 2017.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...