Na Mohamed Ali-Mahakama.

MAHAKAMA ya Tanzania inakusudia kuanzisha kituo cha Mafunzo kwa ajili ya watumishi wake pamoja na wadau ili kuwaongezea ujuzi utakaosaidia kuboresha huduma zinazotolewa na Mahakama. 

Kituo hicho kinachojengwa katika eneo la Mahakama ya Kisutu jijini Dar es salaam kitawaunganisha watumishi wa Mahakama na wadau katika mafunzo kwa njia ya video (video conferencing).

Akizungumzia Kituo hicho, Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof Ibrahim Hamis Juma amesema ujenzi wa kituo hicho ni sehemu ya Maboresho ya huduma za Mahakama ambacho pia wadau wa Mahakama watakuwa ni sehemu ya mafunzo yatakayokuwa yakitolewa.

Amesema badala ya Majaji, Mahakimu, watumishi na wadau wa Mahakama kwenda kupata baadhi ya mafunzo kwenye chuo cha Uongozi wa Mahakama- Lushoto (IJA), baadhi ya mafunzo watakuwa wakiyapata katika kituo hicho.
 Mhandisi wa Mahakama ya Tanzania, Khamadu Kitunzi akielezea teknolojia inayotumika kujenga jengo la kituo cha mafunzo cha mahakama leo jijini dar es salaam.
 Kaimu jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati) akiwa na Mwakilishi wa Benki ya dunia nchini, Bella Bird (kulia) na kulia ni jaji kiongozi wa mahakama kuu ya Tanznaia Mhe. Ferdinand Wambali walipotembelea ujenzi wa kituo cha mafunzo cha Mahakama leo jijini Dar es salaam


Picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...