Na Honorius Mpangala 

Ilikuwa ni mwaka 2006 klabu ya Manchester United ilipofanya ujanja kumsainisha John Michael Nchekwube Obinna. Obi kama anavyojulikana na wengi akiwa klabu ya FK Lyn ya Norway alijikuta akiingia tamaa ya kuvaa jezi ya United na kuingia mkataba wa awali bila wakala wake na klabu yake kujua. 
Akili aliyoitumia Obi ni ya wachezaji wetu wa kiafrika ambao wana teswa na ile methali "tamaa mbele mauti nyuma".Akiwa mzaliwa wa mji wa Jos katikati ya Nigeria alianza safari yake ya soka katika klabu ya hapo nyumbani kwao ya Plateau United.
Akiwa Norway Obi alipotea ghafla katika klabu yake na kusemekana kuwa ametekwa. Kumbe iligundulika alikuwa na Watu wa Manchester United ndipo alifanya 'uswahili' wa kusaini kandarasi ya kuitumikia United. Baadae picha zikasambaa kwenye mitandao akiwa na jezi ya United.
Kwa mapungufu yaliyofanywa na United iliwafanya Chelsea,kupita njia halali ya kumsajili. Uhalali na uwazi walioutumia Chelsea ukaonekana kuwa Manchester walimlazimisha Obi na kutokana na ukubwa wa klabu yao alijikuta anashindwa kukataa kuichezea klabu yao.
Baada ya sakata kufikishwa mbele ya Uefa maamuzi yanatolewa kuwa Manchester United walimsajili Obi kwa njia zisizo sahihi. Hawakumtumia wakala wake walimteka kijana wa watu lakini katika mazingira ambayo hata klabu yake inasemekana walijua ila hawakutaka kuwa wawazi. Maamuzi yalimnufaisha Chelsea na hatimaye Obi mwenyewe kwa kinywa chake akasema nataka kucheza Chelsea na sio Manchester United. Akakazia kuwa huko nilisaini kwa kushinikizwa.
Kwa habari zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...