JUMLA ya nchi Sita leo zimeanza mchuano mkali katika mashindano ya gofu ya kanda ya tano ya Afrika yaliaonza kutimua vumbi katika Viwanja vya Gymkhana, jijini Dar es Salaam.

Mashindano hayo ya siku tatu yaliyoanza jana yanazishirikisha nchi za Rwanda,Burundi,Ethiopia,Uganda, Kenya na wenyeji Tanzania. Katika mchezo uliochezwa jana upande wa ‘Singel’s kati ya Amani saidi kutoka Tanzania na John Karicho kutoka Kenya wachezaji hao walitoka sare katika mashimo 18 waliyocheza. 

Akizungumza baada ya mchuano huo kumalizika, Karicho kutoka Kenya, alisema kuwa mchuano ulikuwa mzuri na wenye upinzani mkubwa kutokana jinsi alivyokuwa nyuma kwa viwanja 3-0 kati ya viwanja 9 walivyocheza. 

Aidha Karicho, alisema kuwa uchezaji wa mpinzani wake, Saidi ni mzuri sana na katika mchezo huo alidai alicheza kwa uangalifu mkubwa katika viwanja 9 vya mwisho kuhakikisha anasawazisha matokeo hayo. 
MCHEZAJI wa Timu ya Gofu ya Tanzania, Amani Said, akipiga mpira katika Shimo Namba 9, wakati akichuana na mpinzani wake John Karichu, kutoka nchini Kenya, katika mashindano ya Tano ya Kanda ya Afrika Mashariki yanayoshirikisha Nchi Sita za Tanzania, Ethiopia, Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda, yaliyoanza jana katika Viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya mashabiki wa mchezo huo waliofika kushuhudia mchuano huo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...