Jonas Kamaleki- MAELEZO.
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi ameridhia mwekazi kupewa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda kijijini Msoga, Wilayani Chalinze, Mkoa wa Pwani.

Waziri Lukuvi amesema kuwa wanakijiji wana uwezo wa kutoa ardhi hadi ekari hamsini tu zaidi ya hapo ni Mhe. Rais mwenye uwezo wa kutoa hati kwa mwekazaji, hivyo alikwenda Msoga kujiridhisha kabla ya kumshauri  Rais kutoa hati kwa mwekezaji.

Aliwauliza wananchi katika mkutano uliofanyika kijijini Msoga kama walikubaliana kumruhusu mwekazaji wa Region Recycling East Africa Limited kujenga kiwanda kijijini hapo, nao wananchi kwa pamoja walisema kuwa ndiyo walitoa ardhi yao kwa ajili ya uwekezezaji huo.

Kiwanda hicho kitakuwa kinatumia betri mbovu za gari na za umeme jua  (Recycling) kama malighafi ya kutengeneza betri nyingine kwa ajili ya matumizi ya magari na mitambo ya umeme jua. Mwekezaji huyo alipewa jumla ya ekari 56 na wanakijiji wa Msoga kwa ajili ya uwekezaji huo.

“Vijiji vilivyopimwa kimji vitaiingizia Serikali mapato na wananchi pia watapata fursa za kupata mikopo kwenye mabenki na kufanya biashara kubwa,”alisema Lukuvi na kuongeza kuwa anazishauri Halmashauri zote nchini kupandisha hadhi vijiji vya namna hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...